Wakati Tanzania ikiadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika Kila Disemba 9 ya mwaka Wananchi mkoani Njombe wameshiriki kufanya usafi wa mazingira na kutoa misaada kwa wagonjwa huku wito ukitolewa kwa jamii kujijengea utamaduni wa kuwa safi wakati wote.
Blog hii Nikwa ajili ya Habari na Matukio Mbalimbali ya Kijamii pamoja na Habari Mchanganyiko
Monday, 9 December 2024
USAFI WAFANYIKA MIAKA 63 YA UHURU WA TANGANYIKA NJOMBE
Wednesday, 4 December 2024
NYUMBA 9 MJI MWEMA NJOMBE ZAEZULIWA NA MVUA KUBWA
Katibu
tawala Wilaya Njombe Bi. Agatha Mhaiki ametoa pole kwa wakazi wa Mtaa wa Mji
Mwema eneo la Msete kwa maaafa ya kuezuliwa nyumba iliyosababishwa na mvua kubwa iliyo nyesha Disemba 03,2024.
Akizungumza
Katibu tawala akiwa eneo la tukio hilo Disemba 04 ,2024 alipoongoza na kamati
ya Ulinzi na Usalama Wilaya Njombe amesema serikali tayari imefanya tathimini
kwa nyumba zilizo pata maafa kwa ajili ya ukamilishaji wa Nyumba hizo kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali.
Akiendelea
kuzungumza na wakazi hao Mhaiki amesema
kwa niabaya ya kamati ya ulinzi na usalama wamechangia shilingi laki tatu tu(300,000)kwa
ajili ya wahanga hao huku taratibu zingine za ukusanyaji zikiendelea.
Kwa Upande
wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe Erasto Mpete amsema taratibu
za uchangiaji zitaratibiwa na ofisi ya Mtendaji wa kata na Mtaa ili kuhakikisha
matumizi ya fedha ambazo watakuwa wamezitoa wadau kutoka maeneo mbalimbali
ziwekwe kwenye kwenye akaunti ya Mtaa
ambayo ni 6062300658 -Mtaa wa Mji Mwema ili kuepusha changamoto katika ukusanyaji.
Jumla ya Nyumba
10 Katika Mtaa wa Mji Mwema zimeezuliwa na Mvua kubwa iliyo nyesha Disemba 03,2024 ambayo
ilisababisha maafa hayo.
WAFANYA BIASHARA SOKO KUU NJOMBE WAPATIWA ELIMU YA MATUMIZI YA DAWA NA VIFAA TIBA
Wafanya Biashara wa Soko Kuu Njombe na soko la wakulima Halmashauri ya mji Njombe wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya dawa na vifaa tiba kwa kutoka mamlaka ya dawa na vifaa tiba.
Akizungumza Disemba 04,2024 Maria Sanga Afisa Elimu kwa Umma kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Nyada za Juu Kusini na wafanyabiashara hao kuhakikisha wanatumia dawa kwa usahihi kama mtaalamu anavo elekeza dawa hizo.
“Kumekuwepo na wimbi la wananchi kutumia dawa pasipo vipimo vya daktari, kutomaliza dawa kwa muda sahihihi na wengine kutumia dawa za binadamu kwenye mifugo niwaombe mkipata changamoto yoyote ya afya na daktari akakwambia tumia dawa hizi kwa muda wa siku kadhaa tumia muda huo kama ulivyo elekezwa usipofanya hivyo unapelekea usugu wa dawa katika mwili wako na kupelekea dawa hiyo kutofanya kazi katika mwili wako ” Alisema Maria Sanga Kutoka TMDA
Akiendelea Kuzungumza Maria amewataka Vijana na Mabinti ambao wamekuwa wakitumia dawa za nguvu za kiume na Dawa za kuua Mbegu za kiume maarufu (P2) zisitumike kilasiku jambo ambalo linaharibu afya zao kutokana namatumizi mabaya ya dawa hizo kinyume na makusudio yake kwa wananchi hasa kwa ambao wamekutana na changamoto .
“Watu wamekuwa wakitumia P2 kila wakifanyapo tendo la Ndoa lakini kitaalamu inatakiwa zitumike mara 2 kwa mwaka na sio kila wakimaliza tendo la ndoa na kwa wanaume dawa za nguvu za kiume zipo kwa wale ambao wanachangamoto za maumbile yao ya mfumo wa uzazi ,sio kwa watu mbao wazima mnajiua wenyewe vijana achene kuwakomoa mabinti mkiamini dawa za nguvu za kiume zinawaridhisha wanawake hapana!!!!. ” Alisema Maria Sanga Kutoka TMDA.
TMDA YAWAFIKIA WAKULIMA WA PARACHICHI NJOMBE
![]() |
Wito huo
umetolewa Disemba 04,2024 na Maria Sanga
Afisa Elimu kwa Umma kutoka Mamlaka
ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Nyada za Juu Kusini ambapo aliwaomba
wakulima na wadau hao wahakikishe wanatumia dawa hizo kama inavyo takiwa kwa
mjibu wa mtaalamu husika ambaye anampa dawa hizo jambo ambalo kwa baadhi ya
watu wanapata usugu wa dawa kutokana na kutumia dawa kwakutozingatia vipimo na
masharti ya daktari.
“Kumekuwepo
na wimbi la wananchi kutumia dawa pasipo
vipimo vya daktari, kutomaliza dawa kwa muda sahihihi na wengine kutumia dawa
za binadamu kwenye mifugo niwaombe
mkipata changamoto yoyote ya afya na daktari akakwambia tumia dawa hizi kwa
muda wa siku kadhaa tumia muda huo kama ulivyo elekezwa usipofanya hivyo unapelekea
usugu wa dawa katika mwili wako na kupelekea dawa hiyo kutofanya kazi katika mwili wako ” Alisema Maria Sanga Kutoka
TMDA
Naye kwa
Upande wake Adam Sorota Mkaguzi wa dawa kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba
(TMDA) Kanda ya Nyada za Juu Kusini amewataka wananchi ambao wata kutana
na changamoto watoe taarifa katika kituo
husika walicho pata dawa hiyo au wawasiliane na Mamlaka husika kwa mawasiliano
ya kupiga namba ya simu bila malipo ya 0800 110 084.
Monday, 2 December 2024
ELIMU YA LISHE YATOLEWA UKUMBINI
AFISA Lishe Mkoa Njombe Betha Nyigu ametumia fursa ya kutoa elimu ya Lishe kwa wananchi walio hudhuria sherehe ya harusi ya Afisa Lishe ajira Mpya (Damiana Danda)Njombe TC.
Katika hafla hiyo aliweza kuwaomba wanachi wote wamkoa njombe kuzingatia elimu lishe,kula makundi yote ya vyakula na kuzingatia mlo kamili kwa mtoto kutokana na ongezeko la udumavu kwa mkoa njombe.
Hafla hiyo pia ilihudhiriwa na maafisa lishe wa Halmashauri zote za mkoa Njombe .
Kujazatumbo sio Lishe
#Lishe ya Mwanao, Mafanikio yake#๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝTulifikisha ujumbe kwa watu zaidi ya 1000#Kujaza tumbo si Lishe, Jali unachomlisha #
AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO
WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...
-
Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii Njombe TC Wapatiwa Mafunzo ya Lishe Kupunguza Udumavu Njombe, Septemba 10, 2025 – Wahudumu wa afya ngazi ya...
-
Novemba 26, 2025 Maafisa ugani Idara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji Njombe wamepatiwa mafunzo na Mradi wa YEFFA kuhusu n...




























.jpg)