Katibu
tawala Wilaya Njombe Bi. Agatha Mhaiki ametoa pole kwa wakazi wa Mtaa wa Mji
Mwema eneo la Msete kwa maaafa ya kuezuliwa nyumba iliyosababishwa na mvua kubwa iliyo nyesha Disemba 03,2024.
Akizungumza
Katibu tawala akiwa eneo la tukio hilo Disemba 04 ,2024 alipoongoza na kamati
ya Ulinzi na Usalama Wilaya Njombe amesema serikali tayari imefanya tathimini
kwa nyumba zilizo pata maafa kwa ajili ya ukamilishaji wa Nyumba hizo kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali.
Akiendelea
kuzungumza na wakazi hao Mhaiki amesema
kwa niabaya ya kamati ya ulinzi na usalama wamechangia shilingi laki tatu tu(300,000)kwa
ajili ya wahanga hao huku taratibu zingine za ukusanyaji zikiendelea.
Kwa Upande
wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe Erasto Mpete amsema taratibu
za uchangiaji zitaratibiwa na ofisi ya Mtendaji wa kata na Mtaa ili kuhakikisha
matumizi ya fedha ambazo watakuwa wamezitoa wadau kutoka maeneo mbalimbali
ziwekwe kwenye kwenye akaunti ya Mtaa
ambayo ni 6062300658 -Mtaa wa Mji Mwema ili kuepusha changamoto katika ukusanyaji.
Jumla ya Nyumba
10 Katika Mtaa wa Mji Mwema zimeezuliwa na Mvua kubwa iliyo nyesha Disemba 03,2024 ambayo
ilisababisha maafa hayo.









No comments:
Post a Comment