Novemba 26, 2025 Maafisa ugani Idara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji Njombe wamepatiwa mafunzo na Mradi wa YEFFA kuhusu namna watakavyo tekeleza mradi unaolenga shughuli za kilimo kwa vijana wa eneo hilo.
Akizungumza wakati akitoa mafunzo hayokatika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe, Luqmaan Kimbute kutoka Shirika la Rikolto amesema mafunzo hayo yamelenga kuongeza uelewa na ujuzi wa wataalamu wa kilimo kuhusu utekelezaji wa mradi wa Ujasiriamali wa Vijana na Mustakabali wa Chakula na Kilimo (YEFFA) ambao utaenda kuwasaidia vijana kujikwamua na maisha na kuongeza kipato katika maisha yao kutokana na wimbi la vijana wengi kutokuwa na ajira
AKiendelea kuzungumza Mtaalamu huyo bwana Luqmaan amesema mradi huo utatekelezwa kwa miaka mitatu ambapo utapanua fursa za ajira kwa vijana katika mnyororo wa thamani wa zao la hilo.
Kupitia ushirikiano kati ya Rikolto, Serikali, sekta binafsi na wadau mbalimbali wa kilimo wakiwemo wakulima (hasa wanawake na vijana), vyama vya wakulima, taasisi za kifedha, watafiti na wanunuzi
wa shirika hilo linaendelea kuchangia mageuzi chanya katika kilimo na mifumo ya chakula.
Mafunzo haya yanatarajiwa kuimarisha ufanisi wa watekelezaji wa mradi na kuleta matokeo chanya kwa jamii ya Njombe na taifa kwa ujumla.








