Wednesday, 4 December 2024

TMDA YAWAFIKIA WAKULIMA WA PARACHICHI NJOMBE

 










Wakulima na Wadau wa Parachichi Halmashauri ya mji Njombe watakiwa kutumia dawa na vifaa tiba kwa usahihi kama matumizi yanavowataka na sio vinginevyo.

Wito huo umetolewa Disemba 04,2024 na Maria Sanga  Afisa Elimu kwa Umma  kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Nyada za Juu Kusini ambapo aliwaomba wakulima na wadau hao wahakikishe wanatumia dawa hizo kama inavyo takiwa kwa mjibu wa mtaalamu husika ambaye anampa dawa hizo jambo ambalo kwa baadhi ya watu wanapata usugu wa dawa kutokana na kutumia dawa kwakutozingatia vipimo na masharti ya daktari.

“Kumekuwepo na wimbi la wananchi  kutumia dawa pasipo vipimo vya daktari, kutomaliza dawa kwa muda sahihihi na wengine kutumia dawa za binadamu kwenye mifugo  niwaombe mkipata changamoto yoyote ya afya na daktari akakwambia tumia dawa hizi kwa muda wa siku kadhaa tumia muda huo kama ulivyo elekezwa usipofanya hivyo unapelekea usugu wa dawa katika mwili wako na kupelekea dawa hiyo kutofanya kazi  katika mwili wako ” Alisema Maria Sanga Kutoka TMDA

Naye kwa Upande wake Adam Sorota Mkaguzi wa dawa kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Nyada za Juu Kusini amewataka wananchi ambao wata kutana na  changamoto watoe taarifa katika kituo husika walicho pata dawa hiyo au wawasiliane na Mamlaka husika kwa mawasiliano ya kupiga namba ya simu bila malipo ya 0800 110 084.

 

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...