Thursday, 12 February 2026

MZIGO WA MIFUKO 150 YA CHOKAA WAPOKELEWA NA WANACHAMA WA TWENDE PAMOJA AMCOS

 MZIGO WA MIFUKO 150 YA CHOKAA WAPOKELEWA NA WANACHAMA WA TWENDE PAMOJA AMCOS

Wanachama wa Twende Pamoja AMCOS Limited wamepokea mzigo wa mifuko 150 ya chokaa utakaotumika kuboresha rutuba ya udongo na kuongeza uzalishaji mashambani.

Makabidhiano ya mzigo huo yalifanyika tarehe 11 Februari 2026, ambapo Mwenyekiti wa Bodi, Todos Leonard Msigwa, alipokea mzigo huo kutoka kwa Emmakrata Kyando, Afisa Masoko wa Guavay Company Limited.

Akizungumza wakati wa mapokezi hayo, uongozi wa AMCOS ulieleza kuwa upatikanaji wa chokaa hiyo ni hatua muhimu katika kukabiliana na changamoto ya tindikali kwenye udongo ambayo imekuwa ikiathiri uzalishaji wa mazao kwa baadhi ya wakulima. Matumizi ya chokaa yanatarajiwa kuongeza rutuba ya udongo, kuboresha afya ya mazao na kuongeza mavuno kwa wanachama.

Aidha, AMCOS imeeleza kuwa itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa pembejeo za kilimo ili kuhakikisha wakulima wanapata huduma na pembejeo bora kwa wakati, hatua itakayosaidia kuongeza tija na kipato kwa wanachama wake.




Monday, 2 February 2026

NJOMBE YAPITIA MBINU SHIRIKISHI ZA KUBORESHA LISHE YA MAMA, WATOTO NA VIJANA BALEHE

 NJOMBE YAPITIA MBINU SHIRIKISHI ZA KUBORESHA LISHE YA MAMA, WATOTO NA VIJANA BALEHE









Tarehe 29 Januari 2026, Mkoa wa Njombe ulifanya kikao cha kupitia na kuchambua mbinu shirikishi za kijamii katika kuboresha lishe ya mama, watoto na vijana balehe. Kikao hicho kililenga kutathmini ufanisi wa afua za lishe zinazotekelezwa na sekta mbalimbali pamoja na kubaini vikwazo vinavyojitokeza katika utekelezaji wake.


Kikao hiki kiliwezeshwa na wadau wa maendeleo CRS na COUNSENUTH kupitia Mradi wa Lishe ya Mwanao, unaofadhiliwa na Serikali ya Norway kupitia UNICEF.


Washiriki wa kikao walitoka katika taasisi na sekta mbalimbali, ikiwemo wataalamu kutoka TAMISEMI, Wizara ya Afya, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wizara ya Elimu pamoja na sekta ya Habari na Mawasiliano.


Aidha, taasisi za utafiti na elimu ya juu zilizoshiriki ni pamoja na SUA, TFNC, MUST, NMIST na Ifakara Health Institute. Mashirika ya kiraia yaliyohudhuria ni TAHEA na SANKU, huku wadau wa maendeleo wakiwemo UNICEF, CRS, COUNSENUTH na CUHAS.


Kwa upande wa Mkoa na Halmashauri, washiriki walijumuisha Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa (Ag. RMO), Kaimu Waganga Wakuu wa Wilaya (Ag. DMOs), Maafisa Lishe, waratibu wa lishe shuleni ngazi ya elimu ya msingi na sekondari, Maafisa Kilimo na Mifugo, walimu wawakilishi, Mratibu wa Wahudumu wa Afya ya Jamii (CHWs) ngazi ya Mkoa pamoja na Afisa Elimu Mratibu wa Lishe ngazi ya Mkoa.


Lengo kuu la kikao hiki lilikuwa kupitia na kuhakiki afua za lishe zinazotekelezwa na sekta mbalimbali ili kubaini ufanisi wake, changamoto zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Lishe (NMNAP) pamoja na kuchangia kufikiwa kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu SDG 2 (Kutokomeza Njaa), SDG 3 (Afya Njema) na SDG 6 (Maji Safi na Usafi wa Mazingira).


@njombe_rs @wizara_afyatz @counsenuth98  @uniceftz @unicef

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...