Thursday, 2 October 2025

WANANCHI MTAA WA KAMBARAGE WAJADILI SHUGHULI ZA MAENDELEO

 Wananchi wa Mtaa wa Kambarage wamekutana kufanya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kujadili shughuli mbalimbali za maendeleo ya mtaa huo.

Lengo kuu la mkutano huu lilikuwa ni kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kushauriana juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Mtaa, Mheshimiwa Fransci Msanga, aliwataka wananchi wote kulinda amani na mshikamano hasa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Aidha, aliwaasa wananchi kushirikiana na viongozi wa mtaa katika masuala ya ulinzi shirikishi ili kuhakikisha usalama unadumishwa.






















Vilevile, Mtendaji wa Mtaa, Ndugu Nicodemas Phuni, aliwahimiza wananchi kuhakikisha wanachangia kwa uaminifu mapato ya mtaa, ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Pia alisisitiza umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika masuala ya afya, lishe bora, usafi wa mazingira na elimu kwa ajili ya kuboresha ustawi wa jamii nzima ya Kambarage.


Kwa pamoja, mkutano uliazimia kuendeleza mshikamano, kuchangia maendeleo, kushirikiana katika usafi wa mazingira na kuhakikisha miradi ya mtaa inakamilika kwa wakati na kwa ufanisi.

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...