Wananchi wa Mtaa wa Kambarage wamekutana kufanya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kujadili shughuli mbalimbali za maendeleo ya mtaa huo.
Lengo kuu la mkutano huu lilikuwa ni kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kushauriana juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Mtaa, Mheshimiwa Fransci Msanga, aliwataka wananchi wote kulinda amani na mshikamano hasa kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Aidha, aliwaasa wananchi kushirikiana na viongozi wa mtaa katika masuala ya ulinzi shirikishi ili kuhakikisha usalama unadumishwa.
Kwa pamoja, mkutano uliazimia kuendeleza mshikamano, kuchangia maendeleo, kushirikiana katika usafi wa mazingira na kuhakikisha miradi ya mtaa inakamilika kwa wakati na kwa ufanisi.



No comments:
Post a Comment