Friday, 24 October 2025

Mgombea Udiwani Erasto Mpete Aahidi Maendeleo kwa Wananchi wa Nole, Kata ya Utalingolo

 













NNa Mwandishi wetu

Oktoba 23, 2025  Mgombea udiwani wa Kata ya Utalingolo, Ndugu Erasto Mpete, ameahidi kuwaletea wananchi wa  Nole maendeleo ya kweli endapo watampa ridhaa ya kuwa mwakilishi wao endapo watamchagua.

Akizungumza mbele ya mamia ya wananchi waliokusanyika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika tarehe 23 Oktoba, Ndugu Mpete alisema dhamira yake kuu ni kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na kujituma, akisisitiza kuwa ataweka kipaumbele katika sekta za elimu, afya, kilimo, umeme, na usafi wa mazingira.


 “Ninawaomba mnitume mimi, mtoto wenu, niwaletee maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Nole. Hayo ndiyo maeneo nitakayoanza nayo mara baada ya kupata ridhaa yenu,” alisema Mpete huku akishangiliwa na wananchi.

Mgombea huyo aliongeza kuwa maendeleo ni mchakato unaohitaji uvumilivu na ushirikiano wa wananchi wote, akihimiza umoja na ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

 “Tuamini kwamba maendeleo si jambo la siku moja. Ni safari inayohitaji ushirikiano, mipango thabiti, na uongozi makini,” alisisitiza.


Mwisho wa hotuba yake, Ndugu Mpete aliwataka wananchi wa Kata ya Utalingolo kujitokeza kwa wingi tarehe 29, siku ya uchaguzi mkuu, na kupiga kura kwa amani, upendo, na umoja, kwa wagombea wanaowaamini kuwa watatetea maslahi ya wananchi.


No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...