Friday, 1 November 2024

Wito watolewa kwa Madiwani kuendelea kusimamia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.

 Wito watolewa kwa Madiwani kuendelea kusimamia  utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.






Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe.Kissa Gwakisa Kasongwa ameendelea kuhimiza madiwani wa Halmashauri ya Mji Mji Njombe, kuhakikisha kuwa wanaendelea kusimamia vizuri miradi yote inayoanza pamoja na ile ambayo haijakamilika (miradi viporo) ili iweze kukamilika katika ubora unaotakiwa na kuanza kuwahudumia wananchi.


Akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Njombe ,Bi.Lilian Nyemele Afisa Tarafa,Tarafa ya Njombe Mjini amesema kuwa ni muhimu kuimarisha ufuatiliaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo ili kuleta manufaa kwa wananchi.


Aidha aliwakumbusha kuwa msimu wa kilimo unakaribia, hivyo ni jukumu la viongozi na wakulima wote kuhakikisha shughuli za kilimo zinafanyika kwa ufanisi  na endapo changamoto yoyote  itajitokeza itolewe taarifa mapema ili kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa chakula.


Katika jitihada za kuboresha afya ya jamii, amewataka wananchi na viongozi kuendelea kuhamasisha umuhimu wa lishe bora sambamba na kushiriki  siku za lishe, akisema kuwa mikakati thabiti ya lishe itasaidia kupunguza tatizo la udumavu kwa watoto na kuimarisha afya za wananchi wote.



Wakati Tanzania ikijiandaa kwa uchaguzi wa serikali za mitaa, Mkuu wa wilaya amesisitiza umuhimu wa kudumisha amani na usalama katika kipindi chote cha uchaguzi. 


Ameitaka jamii ya Njombe kushirikiana kwa karibu na vyombo vya usalama ili kuimarisha amani, kuzuia vurugu, na kuhakikishia kuwa uchaguzi unafanyika kwa utulivu na haki.

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...