Monday, 28 October 2024

MPETE: AWATAKIA WANAFUNZI WOTE WA H/M/NJOMBE MTIHANI MWEMA KIDATO CHA PILI

Oktoba 27 ,2024  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe.Erasto Mpete aliwatakia Mtihani mwema wanafunzi wote wa kidato cha pili Shule ya Sekondari Utalingolo kwa niaba ya Shule zote za Halmashauri ya Mji Njombe ambao tayari wameanza mtihani wao wa  taifa wa upimaji tarehe 28 oktoba hadi tarehe 7 Novemba 2024.


Akiwa katika shule hiyo Mhe Mpete amewaomba wanafunzi hao kufanya vema mitihani hiyo ambayo itakuwa kipimo kikubwa katika taaluma yao ya kuendelea na masomo kidato cha tatu pamoja na kuwasisitiza umakini wawapo katika vyumba vya mitihani.


Mwenyekiti alitoa Peni kwa wanafunzi wote wa kidato cha pili kwa ajili ya mitihani hiyo.



No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...