Kwaya ya Mt. Yudathadei Yaadhimisha Sherehe Kuu kwa Ustadi na Bashasha
Njombe
Katika mwonekano wa kipekee na shauku kubwa ya kusheherekea siku ya Mtakatifu Yudathadei, Kwaya ya Mt. Yudathadei kutoka Parokia ya Njombe imejipambanua kwa kuandaa sherehe maalum ambayo imewakusanya waumini na wakazi wa eneo hilo kwa lengo la kuhamasisha upendo na mshikamano.
Kwa shauku kuu, Mlezi wa Baraza la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Tanzania (NACONGO), Joram Hongoli, aliyehudhuria kama mgeni rasmi, wakati akizungumza na cbknews online ameisifia sana kwaya hii kwa jitihada zao za kipekee katika kuhamasisha jamii kusaidia watoto wenye uhitaji wanaosoma katika shule ya msingi ya Kibena. "Kwaya hii si tu imejikita katika kutangaza neno la Mungu, bali pia imeonesha moyo wa huduma na upendo kwa jamii, jambo ambalo ni mfano wa kuigwa," alisema Hongoli.
Kauli mbiu ya sherehe hii, "Kutakuwepo na changizo kwa ajili ya kuwasadia watoto wenye ulemavu wanaopatikana shule ya msingi Kibena," imeonesha kwa kina moyo wa kutoa ambao kwaya ya Mt. Yudathadei imejiwekea. Mbali na maadhimisho hayo, waimbaji wa kwaya hii watatoa burudani kwa umahiri mkubwa, wakijaza ukumbi na nyimbo za sifa na shukrani, huku nyuso za furaha zikiwa zimetawala kwa waumini wote watakaokuwepo baadae kuanzia saa sita mchana wa leo katika ukumbi wa Jimbo la Njombe.
Kwa namna ya pekee, Kwaya ya Mt. Yudathadei imeendelea kuwa taa ya matumaini kwa jamii ya Njombe, ikiwahamasisha wengi si tu kwa nyimbo zao bali pia kwa shughuli mbalimbali za kijamii wanazozifanya. Ni matumaini ya wengi kuwa moyo huu wa huruma na kujali utaendelea kukua na kuleta mabadiliko chanya zaidi kwa jamii ya Njombe.
Kwa hakika, Kwaya ya Mt. Yudathadei imeonesha kuwa muziki wa injili una nguvu ya kuleta mabadiliko – sio tu rohoni bali pia katika hali halisi ya maisha ya watu. Tunawapongeza na tunawatakia kila la kheri katika juhudi zao za kuendeleza huduma hii takatifu! @radiomariatanzania
✍️Hongera kwa kazi nzuri ya kuunga mkono jamii na kwa kuonesha mfano wa upendo na mshikamano.
.jpg)
No comments:
Post a Comment