Saturday, 26 October 2024

VINCENT MGINA AWAGUSA WANAFUNZI WA KIKE SHULE YA SEKONDARI MADILU

 VINCENT MGINA AWAGUSA WANAFUNZI WA KIKE  SHULE YA SEKONDARI  MADILU.


Mtendaji wa kata ya Madilu Zaveria Mduda kwa kushirikiana na mkazi wa kata hiyo Vincent Mgina wamegawa taulo za kike kwa wanafunzi wa kidato cha pili shule ya Sekondari Madilu wanaotarajia kuanza mitihani yao ya Taifa ya kujipima  ili iwasaidie pale ambapo watakuwa katika mitihani hiyo.


Akizungumza mara baada ya kukabidhi taulo za kike kwa wanafunzi hao oktoba 26 ,2024  Zaveria Mduda  amemshukuru mdau huyo kwa kujitoa  kwa moyo wote  hasa kwakuwagusa wanafunzi hao ,jambo ambalo litaleta hamasa katika kukuza taaluma ya kata hiyo pamoja na kuwafanya wanafunzi kujisikia vizuri wakiwepo shuleni na kuweza kufanya mitihani yao vizuri.































No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...