Thursday, 17 October 2024

TAMISEMI NA VODACOM KUENDELEZA MASHIRIKIANO

 TAMISEMI NA VODACOM KUENDELEZA MASHIRIKIANO


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI Ndugu. Adolf Ndunguru amekutana na wawakilishi kutoka Vodacom Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mpesa Vodacom Tanzania Bw. Epimack Mbeteni ofisini kwake Jengo la Sokoine Jijini Dodoma.


Bw. Nduguru amesema Ofisi yake itaendelea kushirikiana na Vodacom kwa lengo la kuboresha na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi wote.


Naye Bw. Mbeteni  kutoka Vodacom ameahidi kuendeleza ushirikiano kwenye shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa kuwafikia wananchi hasa wa ngazi ya chini kabisa ambako TAMISEMI inafika.


No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...