Oktoba 07,2024 Halmashauri
ya mji Njombe Imesaini mikataba ya ujenzi wa miundombinu ya Shule na Afya na kamapuni
ya Ingenuity works Limited na Hamerkop International Limited.
Akizungumza katika
hafla hiyo Mwenyekiti wa halmashauri ya
mji njombe Mhe Erasto Mpete ameziomba kampuni hizo kwenda kutekeleza miradi hiyo kwa ubora na ufanisi
mkubwa kama ilivyo tarajiwa na wananchi .
“Mhe Rais Dkt .Samia Suluhu Hassan amekuwa akitafuta
fedha kwa nguvu kubwa hivyo anatamani kuona utendaji wa kazi unakuwa kwa
kiwango kikubwa na tunatarajia mnaenda
kufanya kazi kwa utaratibu na miongozo miliyopewa kwa kufanya kazi vizuri ili
kuendana na thamani ya miradi hiyo,imani yangu mtafanya kazi vizuri na kwa unadhifu
mzuri tofauti na mafundi wingine” Alisema Mhe Erasto mpete .
Mikataba hiyo itaenda
kutekeleza Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Wikichi Kata ya Ramadhani kwa
shilingi Milioni 580,Ujenzi wa Mabweni 2 shule ya sekondari Matola kwa shilingi
milioni 280 na Ujenzi wa jengo la Wagonjwa wa Nje ( OPD ) Hospitali ya Kibena Shilingi
milioni 965.









No comments:
Post a Comment