Monday, 7 October 2024

MIKATABA YA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA AFYA NA ELIMU NJOMBE TC YASAINIWA

 


Oktoba 07,2024 Halmashauri ya mji Njombe Imesaini mikataba ya ujenzi wa miundombinu ya Shule na Afya na kamapuni ya Ingenuity works Limited na Hamerkop International Limited.

Akizungumza katika hafla hiyo  Mwenyekiti wa halmashauri ya mji njombe Mhe Erasto Mpete ameziomba kampuni hizo kwenda  kutekeleza miradi hiyo kwa ubora na ufanisi mkubwa  kama ilivyo tarajiwa na wananchi .

“Mhe Rais  Dkt .Samia Suluhu Hassan amekuwa akitafuta fedha kwa nguvu kubwa hivyo anatamani kuona utendaji wa kazi unakuwa kwa kiwango kikubwa na  tunatarajia mnaenda kufanya kazi kwa utaratibu na miongozo miliyopewa kwa kufanya kazi vizuri ili kuendana na thamani ya miradi hiyo,imani yangu mtafanya kazi vizuri na kwa unadhifu mzuri tofauti na mafundi wingine” Alisema Mhe Erasto mpete .

Mikataba hiyo itaenda kutekeleza Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Wikichi Kata ya Ramadhani kwa shilingi Milioni 580,Ujenzi wa Mabweni 2 shule ya sekondari Matola kwa shilingi milioni 280 na Ujenzi wa jengo la Wagonjwa wa Nje ( OPD ) Hospitali ya Kibena Shilingi milioni 965.










No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...