Thursday, 3 October 2024

MEDDA :TWENDENI TUKAJIANDIKISHE UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024

 


Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Mji Njombe Samson Medda amewataka wananchi wote Halmashauri ya mji njombe kuhakikisha wanashiriki  na kujiandikisha kwenye Orodha ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 Novemba 27,2024.

Amesema hayo oktoba 03 ,2024 kwenye kikao kazi cha uwasilishaji wa mpango kazi wa shughuli za maendeleo na kutafsiri 4R za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kata ya njombe mjini kwa mwaka 2024/2025 ambapo Medda amewaomba wakazi wote wa njombe mjini kuhakikisha wanshiriki katika zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa kama 4R za mhe rais zinavo tafsiri.

Aidha Medda ameupongeza uongozi wa kata ya njombe mjini kwa kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kata ya njombe mjini kwa kutokana na miradi mbalimbali kutekelezwa kama vituo vya afya ,madarasa  na Ruzuku za kilimo kwa wakulima.

Alatanga Nyagawa Diwani wa kata ya Njombe Mjini amewaomba wananchi  wa kata hiyo kuendelea kutunza mji kwa usafi wa mazingira .






No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...