Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Mji Njombe Samson Medda amewataka
wananchi wote Halmashauri ya mji njombe kuhakikisha wanashiriki na kujiandikisha kwenye Orodha ya Uchaguzi wa
Serikali za Mitaa 2024 Novemba 27,2024.
Amesema hayo oktoba 03 ,2024 kwenye kikao kazi cha uwasilishaji wa
mpango kazi wa shughuli za maendeleo na kutafsiri 4R za Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kata ya njombe mjini kwa mwaka 2024/2025 ambapo Medda
amewaomba wakazi wote wa njombe mjini kuhakikisha wanshiriki katika zoezi la
uchaguzi wa serikali za mitaa kama 4R za mhe rais zinavo tafsiri.
Aidha Medda ameupongeza uongozi wa kata ya njombe mjini kwa
kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kata ya njombe mjini kwa kutokana na
miradi mbalimbali kutekelezwa kama vituo vya afya ,madarasa na Ruzuku za kilimo kwa wakulima.
Alatanga Nyagawa Diwani wa kata ya Njombe Mjini amewaomba wananchi
wa kata hiyo kuendelea kutunza mji kwa
usafi wa mazingira .
No comments:
Post a Comment