Mtaalamu wa Masuala ya Jamii kutoka Benki Kuu ya Dunia Dkt. Naiman Besta aipongeza halmashauri ya Mji Njombe kwa kutekeleza vema miradi ya kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Shule za Awali na Msingi (BOOST) na Miradi ya Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP)·
Akizunguma Oktoba 01,2024
akiwa katika Shule ya Msingi Mpya ya Mapinduzi kata ya Iwungilo na Shule ya
Sekondari Lunyanywi Dkt Naiman ametoa
pongezi kwa wataalamu na madiwani kwa kusimamia vema ujenzi wa shule hizo mpya.
“Kwa miradi ambayo tumeiona hapa ni ukwelikwamba kunausimaizi mzuri niombe tuendele kumuunga mkono Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan” alisema Dkt. Naiman Besta.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Msaidizi wa Udhibiti Ubora wa Shule, Mwalimu Monica Mpololo, ameongoza ukaguzi
wa miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Mkoa wa Njombe chini ya Mpango wa
Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) na mradi wa BOOST. Ukaguzi huo
ulihusisha maafisa kutoka OR-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,
pamoja na wafadhili kutoka Benki ya Dunia.
Lengo kuu la ukaguzi huu ni kutathmini maendeleo
ya utekelezaji wa miradi inayolenga kuboresha mazingira ya utoaji elimu katika
shule za msingi na sekondari nchini. Miradi inayokaguliwa ni pamoja na ujenzi
wa shule mpya za msingi na sekondari, madarasa ya awali ya mfano, miundombinu
ya elimu, pamoja na ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ili
kuongeza ubora wa elimu nchini.
No comments:
Post a Comment