Thursday, 3 October 2024

Dkt. Naiman Besta:CHANGAMOTO SASA BASI ,PELEKENI WATOTO SHULE






 Mtaalamu wa Masuala ya Jamii kutoka Benki Kuu ya Dunia  Dkt. Naiman Besta aipongeza halmashauri ya Mji Njombe kwa kutekeleza vema miradi ya kuimarisha Ufundishaji na Ujifunzaji kwa Shule za Awali na Msingi (BOOST) na  Miradi ya Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP

 

Akizunguma Oktoba 01,2024 akiwa katika Shule ya Msingi Mpya ya Mapinduzi kata ya Iwungilo na Shule ya Sekondari Lunyanywi  Dkt Naiman ametoa pongezi kwa wataalamu na madiwani kwa kusimamia  vema ujenzi wa shule hizo mpya.












“Kwa miradi ambayo tumeiona hapa ni ukwelikwamba kunausimaizi mzuri niombe tuendele kumuunga mkono Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan” alisema Dkt. Naiman Besta.

Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Udhibiti Ubora wa Shule, Mwalimu Monica Mpololo, ameongoza ukaguzi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa katika Mkoa wa Njombe chini ya Mpango wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) na mradi wa BOOST. Ukaguzi huo ulihusisha maafisa kutoka OR-TAMISEMI, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na wafadhili kutoka Benki ya Dunia.

Lengo kuu la ukaguzi huu ni kutathmini maendeleo ya utekelezaji wa miradi inayolenga kuboresha mazingira ya utoaji elimu katika shule za msingi na sekondari nchini. Miradi inayokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya za msingi na sekondari, madarasa ya awali ya mfano, miundombinu ya elimu, pamoja na ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ili kuongeza ubora wa elimu nchini.



No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...