Trump na Zelensky kukutana huku wanachama wa Republican wakiwa na hasira
Donald Trump amesema atakutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky mjini New York siku ya Ijumaa.
Mgombea huyo wa urais wa chama cha Republican aliambia mkutano wa wanahabari kwamba wawili hao watakutana mwendo wa 09:45 ET (14:45 BST) katika jengo la Trump Tower.
Mkutano huo unatazamiwa kuendelea licha ya ripoti za awali kuwa ulifutwa huku kukiwa na hasira kutoka kwa wana Republican baada ya Zelensky kutembelea jimbo muhimu la Marekani la Pennsylvania.
Siku ya Alhamisi, Zelensky alikutana na Rais wa Marekani Joe Biden na Makamu wa Rais Kamala Harris katika Ikulu ya White House kujadili "mpango wake wa ushindi", ambao anatumai utaishinikiza Urusi kukubali kumalizika kwa vita hivyo kidiplomasia.
Soma zaidi:
Naomi Campbell apigwa marufuku kuwa mdhamini wa shirika la kutoa misaada

Mwanamitindo Naomi Campbell amepigwa marufuku kuwa mdhamini wa shirika moja la kutoa misaada baada ya uangalizi kugundua kuwa fedha za shirika hilo zilitumika katika hoteli za kifahari na kwa huduma za saluni.
Uchunguzi wa Tume ya shirika hilo uligundua kuwa shughuli za maonyesho ya mitindo kwa ajili ya usaidizi hazikufanyika kwa kiasi kikubwa cha pesa kilichopatikana kama ilivyotakiwa.
Badala yake zilitumika kwa ununuzi wa sigara na usalama wa Campbell na malipo mengine ambayo hayajaidhinishwa kwa mmoja wa wadhamini wenzake wa shirika hilo.
"Nimegundua leo kuhusu ugunduzi huo, na nina wasiwasi mkubwa," Campbell, 54, aliliambia shirika la habari la AP.
Aliongeza kuwa yeye sio mtu "aliyekuwa na udhibiti" wa shirika hilo la kutoa misaada.
Ahadi za kuchangisha pesa hazijatekelezwa
Amepigwa marufuku kujihusisha na shirika hilo kwa miaka mitano huku wadhamini wengine wawili, Bianka Hellmich na Veronica Chou, wakipigwa marufuku kwa miaka tisa na minne mtawalia.
Wawakilishi wa mwanamitindo huyo wa Uingereza wamewasiliana na BBC.
Uchunguzi uligundua kuwa malipo yasiyoidhinishwa ya jumla ya £ 290,000 kwa huduma za ushauri yalifanywa kwa Bi Hellmich, ambayo ilikuwa ni ukiukaji wa katiba ya shirika hilo.


No comments:
Post a Comment