Friday, 27 September 2024

Mamlaka ya Lebanon yatoa wito wa kusitishwa kwa mapigano mara moja

 Waziri wa mambo ya nje, Abdallah Bou Habib, amezungumza katika Umoja wa Mataifa na kusema nchi yake inavumilia mzozo unaotishia uwepo wake, na kwamba ilikuwa ni muhimu kuukomesha kabla haujafikia hatua ya kutozuilika.

Hezbollah pia imeashiria kuwa haiko tayari kurudi nyuma, na inaendelea kurusha makombora dhidi ya Israel.

Upande mwingine, Israel imesema itaendelea kuwalenga Hezbollah huku mazungumzo yakiendelea, katika mashambulizi ambayo tayari yameua mamia ya watu kote Lebanon na kuwalazimisha makumi ya maelfu kuyahama makazi yao.

Huku kukiwa na shinikizo kubwa hospitalini na idadi inayoongezeka ya wakazi waliokimbia makazi yao, mamlaka ya Lebanon inaomba kusitishwa kwa mapigano mara moja.



No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...