Friday, 27 September 2024

Mazungumzo ya kusitisha mapigano yataendelea huku mapigano yakiendelea - Netanyahu

 



IDF yadai kuwaua viongozi wengine wakuu zaidi wa Hezbollah katika shambulizi lililopita

Jeshi la Israel linasema kuwa viongozi wakuu waandamizi wa Hezbollah waliuawa wakati wa mashambulizi katika eneo la Beirut siku ya Jumanne.

Katika operesheni waliyoiita "Mishale ya Kaskazini" IDF hapo awali ilisema ilimuua mkuu wa makombora na Kikosi cha Roketi cha Hezbollah - Ibrahim Muhammad Qabisi.

Katika taarifa zake za hivi punde jeshi la Israel linasema wakuu wengine wa kundi hilo waliuawa , akiwemo naibu wa Qabisi.

Wakati hayo yakijiri aubuhi ya leo zimeshuhudiwa picha zinazoonyesha makombora juu ya Haifa yakizuiwa.

Mfumo wa kupambana na makombora wa Iron Dome wa Israel ulikatiza safari za makombora juu ya Haifa, yaliyofyatuliwa kutoka Lebanon.

IDF inasema baadhi ya roketi zimeanguka katika maeneo ya wazi.




#source bbc swahili

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...