IDF yadai kuwaua viongozi wengine wakuu zaidi wa Hezbollah katika shambulizi lililopita
Jeshi la Israel linasema kuwa viongozi wakuu waandamizi wa Hezbollah waliuawa wakati wa mashambulizi katika eneo la Beirut siku ya Jumanne.
Katika operesheni waliyoiita "Mishale ya Kaskazini" IDF hapo awali ilisema ilimuua mkuu wa makombora na Kikosi cha Roketi cha Hezbollah - Ibrahim Muhammad Qabisi.
Katika taarifa zake za hivi punde jeshi la Israel linasema wakuu wengine wa kundi hilo waliuawa , akiwemo naibu wa Qabisi.
Wakati hayo yakijiri aubuhi ya leo zimeshuhudiwa picha zinazoonyesha makombora juu ya Haifa yakizuiwa.
Mfumo wa kupambana na makombora wa Iron Dome wa Israel ulikatiza safari za makombora juu ya Haifa, yaliyofyatuliwa kutoka Lebanon.


No comments:
Post a Comment