Sunday, 29 September 2024

ITULIKE FC NA KIBENA FC WAKABIDHIWA MPIRA /MSHINDI AJINYAKULIA KITITA CHA SHILINGI LAKI MOJA

 



Mbunge wa Jimbo.la Njombe Mjini Mhe. Deo Mwanyika ametoa  shilingi  laki moja kwa Mabingwa wa Mwanyika Cup kata ya Ramadhani huki  na Timu ya Itulike FC wakipewa  shilingi elfu hamsini na mpira mmoja mara  baada ya kushindwa kutamba mbele ya wenyeji wao Itulike FC kwa mikwaju ya penati 4_5.

Akikabidhi zawadi hiyo Septemba 29,2024 Katika Uwanja wa Itulike  kwa niaba ya Mbunge Emilia Mwangeni  Katibu wa Mbunge Jimbo la Njombe  amesema ushirikiano unaotokana na  michezo ndio chachu inayopelekea Mbunge Mwanyika kuendelea kuimarisha michezo Jimboni kwake puamoja na kuboresha miundombinu ya Michezo ambayo amekuwa akiipambania akiwa Bungeni kuhakikisha vijana wananufaika na Michezo kutokana na ajira nyingi zinazotokana na michezo.



Akiendelea kuzungumza katibu wa Mbunge Ndugu Emilia amewaomba Vijana hao kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa serikali za Mitaa kwa kuchukua fomu na kutia nia katika nafasi mbalimbali za Uongozi.

kwa Upande wake Mhe .Nikson Nganyange Diwani wakata ya Ramadhani amesema mashindano hayo yametamatishwa kwa kushuhudia mitanange huo wakukata nashoka ambapo amewaomba vijana na wananchi wa mtaa huo kushiriki katika michezo kutokana na fursa zinazopatikana kypitia Michezo.

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...