Adriano Tunduru (JANGALA) Awasilisha Fomu ya Kugombea Udiwani Kata ya Mji Mwema – Makambako
Mjumbe wa Kamati ya Siasa na kada maarufu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Adriano Tunduru, maarufu kwa jina la JANGALA, ameonesha nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi kwa kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Udiwani katika Kata ya Mji Mwema, Halmashauri ya Mji wa Makambako.
Hatua hii inaonesha dhamira yake ya kuendelea kuwa chombo cha kuwaletea maendeleo wananchi wa Mji Mwema kupitia ushawishi, uzoefu na mchango wake katika siasa na shughuli za kijamii. Tunduru ni mmoja wa viongozi waliowahi kushika nafasi mbalimbali ndani ya chama na anayefahamika kwa uzalendo, uwazi na kusimamia maendeleo ya kweli kwa wananchi.
Wananchi na wanachama wa CCM wamepokea kwa furaha hatua hii ya Jangala, wakionesha matumaini makubwa kuwa atakuwa chaguo sahihi kwa maendeleo ya Kata hiyo, endapo atateuliwa na chama.


No comments:
Post a Comment