Wednesday, 2 October 2024

WANANCHI HAI DC KUNUFAIKA NA ZAO LA PARACHICHI

 






Halmashauri ya Wilaya ya Hai imefanya ziara ya kutembelea  Halmashauri ya Mji Njombe kwa lengo la kujifunza  kilimo cha parachichi na fursa mbalimbali za kiuchumi .

Akizungumza Oktoba 02 ,2024  ulipo wasili ugeni huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Kuruthum Sadick ameishukuru na kuipongeza Halmashauri hiyo kwa kuona fursa mbalimbali  za kilimo cha parachichi katiika halmashauri ya mji njombe ambapo wanachi wengi wamekuwa wakinufaika kupitia zao hilo

“Nimefurahi sana kuona mmekuja kututembelea halmashauri yetu ,naamini hamtatoka kama mlivo kuja  na sisi pia tutajifunza vitu kutoka kwenu ambavyo vitasaidia halmashauri yetu kusonga mbele na kukua zaidi kiuchumi” Alisema Kuruthum Sadick Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe.



Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Hai Mhe.. Edmund Rutaraka
amesema  kwa fursa za kilimo hasa cha parachichi ambazo wameweza kuziona zitaenda kuimarisha uchumi wa wananchi wa hai  kutokana  fursa ambazo wameziona zitakwenda Kunyanyua uchumi wa wawana wilaya hiyo hasa katika kilimo hicho ambacho kimekonga  Nyoyo zao kwa namna wananch wa njombe wanavyo nufaika kwa maelfu ya fedha kupitia kilimo hicho


Halmashauri ya wilaya Hai imetembelea Shamba la Mkulima wa Prachichi Nemes Green Garden , Soko Kuu Njombe namna linavyo fanyakazi  vizuri na  Kiwanda cha kuchakata Parachichi kilichopo Hagafilo kata ya Njombe Mji.

Ziara ya Halmashari ya wilaya ya Hai na Njombe mji italeta mapinduzi makubwa katika uchumi wa wananchi wa halmashauri hizo kwani wataenda kuibua miradi mipya  ambayo itakuwa na tija na yenye ufanisi mkubwa pamoja kuongeza diplomasia chanya ya halmashauri hizo..








No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...