Halmashauri ya Wilaya ya Hai imefanya ziara ya kutembelea Halmashauri ya Mji Njombe kwa lengo la kujifunza kilimo cha parachichi
na fursa mbalimbali za kiuchumi .
Akizungumza Oktoba 02 ,2024 ulipo wasili ugeni huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Kuruthum Sadick ameishukuru na kuipongeza Halmashauri hiyo kwa kuona fursa mbalimbali za kilimo cha parachichi katiika halmashauri ya mji njombe ambapo wanachi wengi wamekuwa wakinufaika kupitia zao hilo
“Nimefurahi sana kuona mmekuja kututembelea halmashauri yetu ,naamini hamtatoka kama mlivo kuja na sisi pia tutajifunza vitu kutoka kwenu ambavyo vitasaidia halmashauri yetu kusonga mbele na kukua zaidi kiuchumi” Alisema Kuruthum Sadick Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya
Wilaya Hai Mhe.. Edmund Rutaraka amesema kwa fursa za
kilimo hasa cha parachichi ambazo wameweza kuziona zitaenda kuimarisha uchumi
wa wananchi wa hai kutokana fursa
ambazo wameziona zitakwenda Kunyanyua uchumi wa wawana wilaya hiyo hasa katika
kilimo hicho ambacho kimekonga Nyoyo zao
kwa namna wananch wa njombe wanavyo nufaika kwa maelfu ya fedha kupitia kilimo
hicho
Halmashauri ya wilaya Hai imetembelea Shamba la
Mkulima wa Prachichi Nemes Green Garden , Soko Kuu Njombe namna linavyo
fanyakazi vizuri na Kiwanda cha
kuchakata Parachichi kilichopo Hagafilo kata ya Njombe Mji.
Ziara ya Halmashari ya wilaya ya Hai na Njombe mji
italeta mapinduzi makubwa katika uchumi wa wananchi wa halmashauri hizo kwani
wataenda kuibua miradi mipya ambayo
itakuwa na tija na yenye ufanisi mkubwa pamoja kuongeza diplomasia chanya ya
halmashauri hizo..







No comments:
Post a Comment