Friday, 27 September 2024

Kwanini kombora hili la masafa marefu linalosifiwa na rais Putin lilikataa kuruka?

 



Kuna uwezekano kulikuwa na ajali mbaya katika kituo cha anga za juu cha jeshi la Urusi, Plesetsk mnamo Septemba 20.

Watafiti na wataalamu wa OSINT wanaamini kwamba kuna uwezekano mkubwa lilikuwa jaribio lisilofaulu la kombora la masafa marefu la RS-28 Sarmat, ambalo inaonekana lililipuka kwenye silo. Kulingana na taarifa zilizopo, BBC imejaribu kuunda upya matukio hayo.

Picha za setlaiti zimeonesha shimo kubwa lililosababishwa na mlipuko katika upande mmoja wa mtambo wa kufyatua kombora hilo. Idhaa ya BBC nchini Urusi ilichunguza picha hizo za setaliti zilizochukuliwa mwezi Julai na Septemba 23 za eneo hilo. Zinaonyesha kuwa sehemu moja ya mtambo wa kufyatua kombora hili iliharibika vibaya

Kwa kuongeza, huduma ya NASA FIRMS , ambayo inafahamisha mara moja kuhusu moto mkubwa duniani kote, iliripoti kuwa mnamo Septemba 20, moto mkali ulionekana kwenye eneo hili.

#source BBCSwahili

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...