Friday, 27 September 2024

Je, maandamano ya Chadema yamefanikiwa?


 Msururu wa maandamano ya kusimamisha shughuli na kutikisa nchi kwa sehemu kubwa yalimaliza wakati wa utawala wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, wingi wa maandamano ya wakati huo – yalikifanya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupachikwa lakabu ya “Chama cha Maandamano” na wapinzani wao wa kisiasa, yaani chama tawala.

Kinachoshuhudiwa sasa ni matangazo makali ya maandamano lakini – maandamano yenyewe hayaji na uzito kama wa wakati ule. Kwa lugha nyingine unaweza kusema haya ya sasa ni ‘maandamano tepetepe.’

Lakini mwitikio mdogo, sio kipimo pekee cha kupima ikiwa maandamano yamefanikiwa au la. Na kabla hatujazama kwenye mjadala huo, kwanza tujiulize katiba ya Tanzania inasemaje kuhusu maandamano.

Mwanasheria Rugemeleza Nshala, ambaye aliwahi kuwa rais wa chama cha wanasheria Tanganyika ameiambia BBC, hatua ya polisi kuzuia maandamano si halali kwani Katiba ya Tanzania, inaruhusu kuandamana, kutoa hisia na kupinga vitu vinavyoonekana kuwa kinyume cha Katiba.

#SourceBBCSwahili

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...