Monday, 30 September 2024

HALMASHAURI YA WILAYA GAIRO WAJA KUJIFUNZA KILIMO CHA PARACHICHI NJOMBE MJI


 


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji njombe Mhe. Erasto mpete ameupokea ugeni kutoka Halamshauri ya Wilaya ya Gairo ambao umekuja kujifunza kilimo cha Parachichi katika Halmashauri ya mji njombe .

Akizungumza Septemba  30,2024 mara baada ya kuupokea ugeni huo  Mhe Mpete amewakaribishwa wageni hao ambapo amewaomba kutembelea mashamba mbalimbali ya wakulima wakubwa na walio fanikiwa kupitia zao hilo ili waweze kujifunza na  kuyapata yale ambayo wanatarajia kupitia zao .

Kwaupande wake Mhe. Rachel Nyangasi Diwani kata ya Chigelana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Gairo amesema lengo la kuja kujifunza kilimo cha parachichi Halmashauri ya Mji Njombe nikutokana na ubora ambao halmashauri ya mji aimekuwa ikitengeneza katika zao hilo hasa kwa kuzingatia ubora ,namna ya Kaunda mashamba ya parachichi na hatau mbalimbali za kuanzishwa kwa mashamba ya zao hilo hadi katika masoko .



Halmashauri ya wilaya ya Gairo wamekuja na wataalamu wa kilimo ,Biashara pamoja na  Waheshimiwa madiwani wa wilaya hiyo ambayo imekuwa ikilima mazao mablimbali hasa alizeti na mahindi.

Na Mwandishi wako Mario Mgimba 

0622467223

 


No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...