NJOMBE YAPITIA MBINU SHIRIKISHI ZA KUBORESHA LISHE YA MAMA, WATOTO NA VIJANA BALEHE
Tarehe 29 Januari 2026, Mkoa wa Njombe ulifanya kikao cha kupitia na kuchambua mbinu shirikishi za kijamii katika kuboresha lishe ya mama, watoto na vijana balehe. Kikao hicho kililenga kutathmini ufanisi wa afua za lishe zinazotekelezwa na sekta mbalimbali pamoja na kubaini vikwazo vinavyojitokeza katika utekelezaji wake.
Kikao hiki kiliwezeshwa na wadau wa maendeleo CRS na COUNSENUTH kupitia Mradi wa Lishe ya Mwanao, unaofadhiliwa na Serikali ya Norway kupitia UNICEF.
Washiriki wa kikao walitoka katika taasisi na sekta mbalimbali, ikiwemo wataalamu kutoka TAMISEMI, Wizara ya Afya, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Wizara ya Elimu pamoja na sekta ya Habari na Mawasiliano.
Aidha, taasisi za utafiti na elimu ya juu zilizoshiriki ni pamoja na SUA, TFNC, MUST, NMIST na Ifakara Health Institute. Mashirika ya kiraia yaliyohudhuria ni TAHEA na SANKU, huku wadau wa maendeleo wakiwemo UNICEF, CRS, COUNSENUTH na CUHAS.
Kwa upande wa Mkoa na Halmashauri, washiriki walijumuisha Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa (Ag. RMO), Kaimu Waganga Wakuu wa Wilaya (Ag. DMOs), Maafisa Lishe, waratibu wa lishe shuleni ngazi ya elimu ya msingi na sekondari, Maafisa Kilimo na Mifugo, walimu wawakilishi, Mratibu wa Wahudumu wa Afya ya Jamii (CHWs) ngazi ya Mkoa pamoja na Afisa Elimu Mratibu wa Lishe ngazi ya Mkoa.
Lengo kuu la kikao hiki lilikuwa kupitia na kuhakiki afua za lishe zinazotekelezwa na sekta mbalimbali ili kubaini ufanisi wake, changamoto zilizopo na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Lishe (NMNAP) pamoja na kuchangia kufikiwa kwa Malengo ya Maendeleo Endelevu SDG 2 (Kutokomeza Njaa), SDG 3 (Afya Njema) na SDG 6 (Maji Safi na Usafi wa Mazingira).
@njombe_rs @wizara_afyatz @counsenuth98 @uniceftz @unicef







No comments:
Post a Comment