Tuesday, 15 July 2025

WARATIBU WA UCHAGUZI WA MIKOA, WASIMAMIZI WA UCHAGUZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA JIMBO, MAAFISA UCHAGUZI NA MAAFISA UNUNUZI WAPATIWA MAFUNZO MAALUM YA UCHAGUZI

 

 

WARATIBU WA UCHAGUZI WA MIKOA, WASIMAMIZI WA UCHAGUZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA JIMBO, MAAFISA UCHAGUZI NA MAAFISA UNUNUZI WAPATIWA MAFUNZO MAALUM YA UCHAGUZI

 


Julai 15,2025, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanza kutoa mafunzo ya siku tatu kwa Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi pamoja na Maafisa Ununuzi. Mafunzo haya yataendelea hadi tarehe 17 Julai 2025.

 

Mafunzo haya ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao, yakilenga kuwawezesha washiriki kuelewa kwa kina majukumu yao, sheria, taratibu na miongozo ya uchaguzi, pamoja na mbinu

 

bora za usimamizi na utekelezaji wa shughuli za uchaguzi kwa kuzingatia misingi ya uhuru, uwazi, haki na ufanisi.

 

Kaulimbiu ya uchaguzi huu ni:

“Kura Yako Haki Yako – Jitokeze Kupiga Kura.”

Kaulimbiu hii inalenga kuhamasisha wananchi wote wenye sifa kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia kwa kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.

 

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi inasisitiza kuwa kupitia mafunzo haya, watendaji wake wataweza kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji, na hivyo kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa huru, wa haki na unaoaminika kwa pande zote.

No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...