WARATIBU WA
UCHAGUZI WA MIKOA, WASIMAMIZI WA UCHAGUZI, WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA JIMBO,
MAAFISA UCHAGUZI NA MAAFISA UNUNUZI WAPATIWA MAFUNZO MAALUM YA UCHAGUZI
Julai 15,2025,
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanza kutoa mafunzo ya siku tatu kwa Waratibu
wa Uchaguzi wa Mikoa, Wasimamizi wa Uchaguzi, Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi
ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi pamoja na Maafisa Ununuzi. Mafunzo haya
yataendelea hadi tarehe 17 Julai 2025.
Mafunzo haya ni
sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao, yakilenga kuwawezesha washiriki
kuelewa kwa kina majukumu yao, sheria, taratibu na miongozo ya uchaguzi, pamoja
na mbinu
bora za
usimamizi na utekelezaji wa shughuli za uchaguzi kwa kuzingatia misingi ya
uhuru, uwazi, haki na ufanisi.
Kaulimbiu ya
uchaguzi huu ni:
“Kura Yako Haki
Yako – Jitokeze Kupiga Kura.”
Kaulimbiu hii
inalenga kuhamasisha wananchi wote wenye sifa kushiriki kikamilifu katika
mchakato wa kidemokrasia kwa kutumia haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.
Tume Huru ya
Taifa ya Uchaguzi inasisitiza kuwa kupitia mafunzo haya, watendaji wake
wataweza kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na uwajibikaji, na hivyo
kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa huru, wa haki na unaoaminika kwa pande zote.
No comments:
Post a Comment