Viongozi
Wapya wa Tiba Asili Njombe Wachaguliwa Njombe TC
![]() |
Njombe,
Julai 23,
2025 –Kundi la wataalamu wa tiba asili wakiongozwa na Dkt. Kusulila, ambaye pia
ni Katibu wa Tiba Asili nchini na Mratibu wa magonjwa ya kifua kikuu na Ukimwi,
Halmashauri ya Mji Njombe limefanya kikao maalum katika ukumbi wa Halmashauri
ya Mji wa Njombe, ambapo viongozi wapya wa kundi hilo walichaguliwa rasmi.
Kikao
hicho kilihudhuriwa na waganga wa tiba asili kutoka maeneo mbalimbali ya Halmashauri
ya mji njombe na kuwezeshwa na uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, chini
ya Katibu wa Halmashauri hiyo. Kikao kililenga kuimarisha mwelekeo wa huduma za
tiba asili sambamba na kanuni za kiafya na maadili ya taaluma hiyo.
Dkt.
Kusulila alieleza kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuwa na mifumo ya usimamizi
thabiti kwa waganga wa tiba asili, ili kuhakikisha wanatoa huduma salama na
zinazozingatia taratibu za afya. Alisisitiza kuwa tiba asili inapaswa
kushirikiana na huduma za kisasa, hasa katika mapambano dhidi ya magonjwa sugu
kama Ukimwi na kifua kikuu.
“Tunataka
kuondoa matabibu wa kiholela na kuhakikisha kila mganga wa tiba asili
anasajiliwa, anapata mafunzo, na anashirikiana na sekta rasmi ya afya. Hii
itasaidia kulinda wananchi dhidi ya madhara na kukuza tiba asili kwa njia ya
kitaalamu,” alisema Dkt. Kusulila.
Kwa upande
wake, Katibu wa Halmashauri ya Mji wa Njombe alitoa wito kwa waganga wa tiba
asili kufanya kazi kwa kushirikiana
na
serikali na kuzingatia sheria. Aliahidi kuwa halmashauri itaendelea kutoa
ushirikiano wa karibu kwa kuhakikisha kuwa huduma za tiba asili zinatambuliwa
na kusimamiwa ipasavyo.
Viongozi
walioteuliwa katika kikao hicho watawajibika katika kusimamia usajili wa
waganga, nidhamu, na kuandaa mikakati ya maendeleo ya tiba asili kwa mkoa wa
Njombe.






No comments:
Post a Comment