Serikali mkoani Njombe imepiga marufuku wananchi kutupa makopo ya maji au ya soda barabarani na kwenye mifereji na badala yake wayahifadhi katika vifaa maalumu yakiwemo Mapipa,Mifuko na ndoo ili kuweka mazingira katika hali ya usafi.
Katika Maadhimisho ya siku ya Skauti Duniani,Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe, Bi Agatha Mhaiki kwa niaba ya mkuu wa mkoa anawataka wajasiriamali kuzingatia usafi wakati wa uuzaji wa juisi huku wananchi wakitakiwa kuacha tabia ya kutupa makopo njiani.
Ofisa Afya mkoa wa Njombe Saada Milanzi anasema licha ya Skauti kuadhimisha siku yao kwa kufanya usafi katika mtaa wa Idundilanga Mjini Njombe lakini Serikali inaendelea kusisitiza Wananchi kufanya usafi kila Juma Mosi ya mwisho wa mwezi.
No comments:
Post a Comment