Saturday, 1 March 2025

SERIKALI MKOANI NJOMBE IMEPIGA MARUFUKU WANANCHI KUTUPA MAKOPO YA MAJI AU YA SODA BARABARANI

 Serikali mkoani Njombe imepiga marufuku wananchi kutupa makopo ya maji au ya soda barabarani na kwenye mifereji na badala yake wayahifadhi katika vifaa maalumu yakiwemo Mapipa,Mifuko na ndoo ili kuweka mazingira katika hali ya usafi.




Katika Maadhimisho ya siku ya Skauti Duniani,Katibu Tawala wa Wilaya ya Njombe, Bi Agatha Mhaiki kwa niaba ya mkuu wa mkoa anawataka wajasiriamali kuzingatia usafi wakati wa uuzaji wa juisi huku wananchi wakitakiwa kuacha tabia ya kutupa makopo njiani.

Ofisa Afya mkoa wa Njombe Saada Milanzi anasema licha ya Skauti kuadhimisha siku yao kwa kufanya usafi katika mtaa wa Idundilanga Mjini Njombe lakini Serikali inaendelea kusisitiza Wananchi kufanya usafi kila Juma Mosi ya mwisho wa mwezi.

Aidha wananchi wa Mjini Njombe mara baada ya kushiriki zoezi la usafi majira ya asubuhi wamesema suala la usafi ni tabia ya mtu hivyo wananchi wenye tabia ya kutoa taka nyumbani na kuzitelekeza kwenye makazi ya watu wanapaswa kukoma mara moja.

Maadhimisho ya Siku ya Skauti Duniani, ambayo hufanyika Machi 1  kila mwaka   yalianza kwa kufanya usafi wa mazingira kata ya Njombe Mjini na kuhitimishwa kwa kuzungumza na wananchi  wa Mtaa wa Idundilanga walioshiriki katika shughuli za usafi wa mazingira.










No comments:

Post a Comment

AKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO

  WAKULIMA WA CHAI NJOMBE WAIBUA CHANGAMOTO ZA MIUNDOMBINU NA SOKO Wakulima wa zao la chai mkoani Njombe wameiomba serikali pamoja na wada...